Matthew 16:1-6

Mafarisayo Wadai Ishara

(Marko 8:11-13; Luka 12:54-56)

1 aMafarisayo na Masadukayo wakamjia Isa na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.

2 bIsa akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’ 3 cNanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati. 4 dKizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Isa akawaacha, akaenda zake.

Chachu Ya Mafarisayo Na Masadukayo

(Marko 8:14-21)

5 eWanafunzi wake walipofika ng’ambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate. 6 fIsa akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”

Copyright information for SwhKC